Na Rehema Lucas, DAR ES SALAAM
BEKI wa kati wa Simba, Abdi Banda amesimamishwa kwa muda usiojulikana kucheza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa kosa la kumpiga ngumi kiungo wa Kagera Sugar, George Kavilla katika mchezo wa ligi hiyo baina ya timu hizo Aprili 2, Uwanja wa Kaitaba Bukoba.
Hayo yamefikiwa na Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji wa Ligi Tanzania au Kamati ya Saa 72, katika kikao chake cha juzi mjini Dar es Salaam.
Katika mchezo huo namba 194, ambao Kagera Sugar waliifunga Simba 2-1, Banda aliyekuwa amevalia jezi namba 24 amesimamishwa kucheza Ligi Kuu wakati akisubiri suala lake la kumpiga ngumi George Kavilla aliyevalia jezi namba 15 akiwa hana mpira kusikilizwa na kutolewa uamuzi na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Abdi Banda amesimamishwa kwa muda usiojulikana kucheza Ligi Kuu kwa kosa la kumpiga ngumi George Kavilla wa Kagera Sugar
Kama pia ilibaini Banda ambaye hakupewa adhabu yoyote na refa kwa sababu hakuona tukio hilo, alifanya kitendo cha aina hiyo kwenye mechi namba 169 kati ya Simba na Yanga iliyofanyika Februari 25, 2017 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam akimpiga kiungo Said Juma ‘Makapu’.
Awali, Klabu ya Kagera Sugar iliwasilisha malalamiko dhidi ya kitendo cha beki wa Simba, Abdi Banda kumpiga ngumi kiungo wao George Kavilla wakati akiwa hana mpira, na Mwamuzi wa mechi hiyo kutochukua hatua yoyote.
Kwa vile kosa hilo ni la kinidhamu, Kamati imemsimamisha Abdi Banda kwa mujibu wa Kanuni ya 9 (5) wakati akisubiri suala lake kusikilizwa na kutolewa uamuzi na Kamati ya Nidhamu ya TFF. Kamati ya Nidhamu inatarajiwa kukaa wakati wowote wiki ijayo.
Kamati ya Saa 72 pia imeagiza Daktari wa Uwanja wa Kambarage, Shinyanga, Dk. Abel Kimuntu apelekwe Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya hatua za kinidhamu kutokana na kukataa kuwasilisha taarifa yake kuhusu tuhuma za kupuliziwa dawa kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha Majimaji katika mechi namba 170 ya Ligi Kuu ya Vodacom dhidi ya wenyeji Stand United.
Majimaji iliwasilisha malalamiko yake kwa Bodi ya Ligi kuhusu suala hilo na Kamati ikaagiza ripoti ya daktari huyo ambaye amekataa kutoa ushirikiano kwa mwendeshaji wa Ligi juu ya jambo hilo.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2of4hTE
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang ABDI BANDA ASIMAMISHWA KWA UBONDIA. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2017/04/abdi-banda-asimamishwa-kwa-ubondia.html. Terimakasih atas perhatiannya.