Na Rehema Lucas, DAR ES SALAAM
KIPA namba moja Tanzania, Aishi Salum Manula amempongeza kipa wa pili, Said Mohammed Mduda baada ya jana kuisaidia Taifa Stars kuchukua nafasi ya tatu katika michuano ya COSAFA Castle nchini Afrika Kusini.
Taifa Stars imechukua nafasi ya tatu Kombe laa COSAFA Castle usiku wa jana baada ya ushindi wa penalti 4-2 dhidi ya Lesotho kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 usiku huu Uwanja wa Moruleng mjini Rusternburg na kupitia akaunti yake ya Instagram kipa mpya wa Simba, Manula anayetokea Azam FC amempongeza Mduda.
Kipa Said Mohammed Mduda jana alipangua penalti ya Nahodha wa Lesotho, Thapelo Mokhehle kuipa Tanzania ushindi wa tatu COSAFA
“Hakika wewe ni bora kaka, na mara zote umekuwa bora. Kazi uliyoifanya leo ni kubwa mno kwetu Watanzania. Pia unastahili kupewa pongezi kwa ulichofanya. Kwangu mimi wewe ndiye Mchezaji Bora wa Mechi na ulistahili kaka, endelea hivyo hivyo,”alisema Manula jana baada ya mechi.
Kipa huyo wa Mtibwa Sugar ya Morogoro aliyewahi kudakia Yanga ya Dar es Salaam na Maji Maji ya Songea, alikuwa shujaa jana Taifa Stars baada ya kupangua penalti ya Nahodha wa Mamba, Thapelo Mokhehle kufuatia Sera Motebang kugongesha mwamba wa kulia mkwaju wake na kurudi uwanjani.
Waliofunga penalti za Lesotho ni Hlompho Kalake na Tsoanelo Koetle wakati Shiza Kichuya aligongesha mwamba wa juu penalti ya kwanza ya Tanzania, kabla ya Nahodha Himid Mao,Simon Msuva, Abdi Banda na Raphael Daudi kumtungua kipa wa Mamba Samuel Ketsekile kuipatia Taifa Stars ushindi mzuri wa 4-2.
Aishi Manula (kushoto) amempongeza Said Mohammed (kulia) kwa kazi ya jana Kombe la COSAFA Castle
Ushindi unakuja siku 25 baada ya timu hizo kutoka sare ya 1-1 Juni 10, mwaka huu katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi L kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Kutoka na ushindi huo, Tanzania inaondoka na dola za Kimarekani 10,000 zaidi ya Sh. Milioni 22 kwa fedha za nyumbani, wakati Lesotho wamepata dola 8,300.
Fainali ya COSAFA Castle 2017 itachezwa Jumapili Uwanja wa Royal Bafokeng, Phokeng mjini Rusternburg baina ya majirani, Zambia na Zimbabwe na bingwa atapata dola 42,000 na mshindi wa pili dola 21,000.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2uB9IgR
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang MANULA ‘AMVULIA KOFIA’ SAID MOHAMMED MDUDA KWA KAZI YA JANA. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2017/07/manula-amvulia-kofia-said-mohammed_7.html. Terimakasih atas perhatiannya.