Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
TANZANIA imefanikiwa kushika nafasi ya tatu katika michuano ya COSAFA Castle baada ya ushindi wa penalti 4-2 dhidi ya Lesotho kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 usiku huu Uwanja wa Moruleng mjini Rusternburg, Afrika Kusini.
Shujaa wa Taifa Stars leo amekuwa golikipa Said Mohammed Mduda aliyepangua penalti ya Nahodha wa Mamba, Thapelo Mokhehle baada ya Sera Motebang kugongesha mwamba wa kulia mkwaju wake na kurudi uwanjani.
Waliofunga penalti za Lesotho ni Hlompho Kalake na Tsoanelo Koetle wakati Shiza Kichuya aligongesha mwamba wa juu penalti ya kwanza ya Tanzania, kabla ya Nahodha Himid Mao,Simon Msuva, Abdi Banda na Raphael Daudi kumtungua kipa wa Mamba Samuel Ketsekile kuipatia Taifa Stars ushindi mzuri wa 4-2.
 |
| Nahodha wa Tanzania, Himid Mao (kulia) akiweka mpira kifuani mbele ya kiungo wa Lesotho, Napo Matsoso (kushoto) leo Uwanja wa Moruleng mjini Rusternburg, Afrika Kusini |
 |
| Kipa Said Mohammed amepangua penalti ya Nahodha wa Lesotho, Thapelo Mokhehle kuipa Tanzania ushindi wa tatu COSAFA |
Ushindi unakuja siku 25 baada ya timu hizo kutoka sare ya 1-1 Juni 10, mwaka huu katika mchezo wa ufunguzi wa Kundi L kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Romeo Kasengele wa Zambia, aliyesaidiwa na washika vibendera Thomas Kusosa wa Zimbabwe na Helder de Carvalho wa Angola, ndani ya dakika 90 timu hizo zilishambuliana kwa zamu, Lesotho wakitawala zaidi kipindi cha kwanza na cha pili Taifa Stars wakazinduka.
Kutoka na ushindi huo, Tanzania inaondoka na dola za Kimarekani 10,000 zaidi ya Sh. Milioni 22 kwa fedha za nyumbani, wakati Lesotho wamepata dola 8,300.
Fainali ya COSAFA Castle 2017 itachezwa Jumapili Uwanja wa Royal Bafokeng, Phokeng mjini Rusternburg baina ya majirani, Zambia na Zimbabwe na bingwa atapata dola 42,000 na mshindi wa pili dola 21,000.
Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Said Mohammed, Shomary Kapombe, Gardiel Michael, Nurdin Chona, Salim Mbonde/Abdi Banda dk61, Salmin Hoza/Muzamil Yassin dk61, Himid Mao, Simon Msuva, Raphael Daudi, Stahmili Mbonde/Elias Maguri dk71 na Shiza Kichuya.
Lesotho; Samuel Ketsekile, Itumeleng Falene, Motlomelo Mkwanazi, Thapelo Mokhehle, Bokang Sello, Kefuce Mahula/ Hlompho Kalake dk89, Tumelo Khutlang, Tsoanelo Koetle, Napo Matsoso, Jane Ntso/ Mabuti Potloane dk59 na Sera Motebang.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2uzr7Gx
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang TAIFA STARS WABEBA DOLA 10,000 COSAFA. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2017/07/taifa-stars-wabeba-dola-10000-cosafa.html. Terimakasih atas perhatiannya.