Na Mwandishi Wetu, MBEYA
KIUNGO wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Geoffrey Bonny Namwandu (37) amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kusumbuliwa na maradhi kwa muda mrefu.
Dada wa mchezaji huyo wa zamani wa Prisons ya Mbeya na Yanga SC ya Dar es Salaam, Neema ameiambia Bin Zubeiry Sports – Online leo kwamba wamempoteza kipenzi chao baada ya kuhangaika naye kumuuguza kwa muda mrefu.
Neema amesema kwamba msiba upo nyumbani kwao mjini Mbeya ambako taratibu za mazishi zimekwishaanza.
Geoffrey Bonny hali yake ilivyokuwa siku za mwisho za uhai wake
Bonny alikuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars enzi za kocha Mbrazil, Marcio Maximo na wengi wanamkumbuka kwa soka yake maridadi katika sehemu ya kiungo, licha ya kwamba aliibuliwa wakati umri wake umekwishaenda.
Alicheza Yanga chini ya kocha Mserbia, Profesa Dusan Kondic na akaendelea hata alipoondolewa mwalimu huyo na kuletwa Mseribia mwingine, Kostadin Papic.
Timu ya mwisho ya Geoffrey Bonny kuchezea, Simrik SYC ya Nepal
Geoffrey Bonny (wa pili kulia waliosimama) akiwa kwenye kikosi cha Simrik SYC ya Nepal. Wa pili kushoto waliosimama ni mchezaji mwingine wa Tanzania, Pius Kisambale
Geoffrey Bonny akiichezea Taifa Stars kwenye michuano ya CHAN mwaka 2009
Ni kati ya wachezaji walioiwezesha Taifa Stars kukata tiketi ya kucheza fainali pekee za michauno ya Ubingwa wa Afrika (CHAN) zinazohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee.
Hata hivyo, Maximo akamtema katika kikosi cha Stars baada ya fainali za CHAN nchini Ivory Coast mwaka 2009 kutokana na kuwa majeruhi.
Maumivu hayo yalimfanya aachwe na Yanga mwaka 2011 akaenda kumalizia soka yake Simrik SYC ya Nepal.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2kPQIWI
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang
. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2017/02/na-mwandishi-wetu-mbeya-kiungo-wa.html. Terimakasih atas perhatiannya.