Na Rehema Lucas, DAR ES SALAAM
SIMBA SC imekwenda leo kambini visiwani Zanzibar kujiandaa na mchezo dhidi ya mahasimu, Yanga Jumamosi ya wiki ijayo, huku Nahodha Jonas Gerald Mkude akisema watashinda mechi hiyo.
Simba watakutana na watani wa jadi, Yanga Februari 25, mwaka huu katika mchezo wa marudiano wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na leo wameondoka kwa boti kwenda Zanzibar kwa kambi ya wiki moja.
Mechi mbili zilizopita za Ligi Kuu dhidi ya Yanga, Simba iliweka kambi Chuo cha Biblia, Bigwa mkoani Morogoro na baada ya kufungwa 2-0 na kutoa sare ya 1-1 sasa wanarejea Zanzibar.
Kocha Joseph Omog (kulia) akizungumza na Msaidizi wake, Jackson Mayanja wakati wa safari ya Zanzibar leo
Nahodha wa Simba, Jonas Gerald Mkude alisema jana kwamba hadi sasa wako vizuri kuelekea mchezo huo wa Februari 25.
“Yanga ni timu kama timu nyingine, wao wanajiandaa na sisi tunajiandaa na wachezaji wote wako vizuri na dakika 90 ndizo zitakazoongea,”alisema.
Simba inakwenda kambini Zanzibar siku moja baada ya kutinga Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC) kufuatia kuifunga 1-0 African Lyon jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, bao pekee la Laudit Mavugo.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Burundi, alifunga bao hilo dakika ya 57 baada ya kumzidi maarifa beki wa Lyon, Hassan Isihaka na kufumua shuti dhaifu lililompita kipa Mcameroon, Rostand Youthe kufuatia pasi ya mshambuliaji Ibrahim Hajib.
Kikosi cha Simba kichoingia kambini leo kinaundwa na makipa; Daniel Agyei, Peter Manyika na Dennis Richard.
Mabeki Janvier Bokungu, Hamad Juma, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Vincent Costa, Novaty Lufunga na Method Mwanjali.
Viungo ni Jonas Mkude, James Kotei, Said Ndemla, Mohammed ‘Mo’ Ibrahim, Muzamil Yassin, Mwinyi Kazimoto, Shiza Kichuya na Jamal Mnyate.
Washambuliaji ni Laudit Mavugo, Pastory Athanas, Ibrahim Ajibu, Hijja Ugando na Juma Luizio.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2kxA81t
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms