Na Rehema Lucas, DAR ES SALAAM
KIKOSI cha wachezaji 25 wa Everton kimewasili mjini Dar es Salaam asubuhi ya leo tayari kwa mchezo maalum wa kirafiki na Gor Mahia ya Kenya kesho Uwanja wa Taifa, lakini kiungo Ross Barkley hayumo baada ya kuachwa kutokana na kuwa majeruhi.
Everton imesema kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 anasumbuliwa na maumivu ya nyonga na hayumo katika orodha ya nyota 25 waliotua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam.
Miongoni mwa nyota waliowasili asubuhi ya leo na kupokewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe baada ya safari ya tangu usiku wa jana walipoondoka Uwanja wa Ndege wa Liverpool, ni wachezaji mpya Wayne Rooney, Michael Keane na Davy Klaassen.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akisalimiana na mchezaji wa Everton, Wayne Rooney baada ya kuwasilia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam asubuhi ya leo
Barkley anaingia katika mwaka wa mwisho wa mkataba wake, lakini hatasaini mkataba mpya na kocha wa Everton, Ronald Koeman anaamini Barkley atauzwa kama hatasaini, kwani umuhimu wake umepungua baada ya kuwasili kwa Rooney na Klaassen, pamoja na Gylfi Sigurdsson — wachezaji wote ambao wanaweza kucheza nafasi yake.
Wachezaji waliowasili ni Jordan Pickford, Sandro Ramirez, Wayne Rooney, Kevin Mirallas, Aaron Lennon, James McCarthy, Idrissa Gana Gueye, Gareth Barry, Davy Klaassen, Muhamed Besic, Maarten Stekelenburg, Morgan Schneiderlin, Leighton Baines, Michael Keane, Ashley Williams, Phil Jagielka, Yannick Bolasie, Seamus Coleman, Ramiro Funes Mori, Tom Davies, Dominic Calvert-Lewin, Mason Holgate, Ademola Lookman, Joel Robles, Oumar Niasse, Matthew Pennington, Jonjoe Kenny na Joe Williams.
Mchezo huo utakaoanza Saa 11:00 jioni, utachezeshwa na refa maarufu nchini, Israel Mujuni Nkongo, wakati mgeni Rasmi atakuwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan.
Gor Mahia ilipata nafasi ya kucheza na Everton baada ya kuibuka bingwa wa michuano ya SportPesa Super Cup, ikiwafunga mahasimu, AFC Leopards 3-0 katika fainali ya timu za Kenya tupu baada ya timu za wenyeji zote, Simba, Yanga na Singida United kutolewa mapema.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2u7Fl4c
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms