Na Innocent Okama, KIGALI
TANZANIA wanamenyana na wenyeji, Rwanda leo katika mchezo wa ushindani na upinzani mkali kuwania kusogea hatua ya mwisho ya mtoano wa kupigania tiketi ya Fainali za Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN) mwakani nchini Kenya, michuano inayoshirikisha wachezaji wanaocheza nchini mwao pekee.
Timu hizo zitateremka katika Uwanja wa Kigali, maarufu kama Nyamirambo katika mchezo utakaoanza Saa 9:30 kwa Saa za Rwanda zikitoka kutoa sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza Jumamosi iliyopita Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
Maana yake, Taifa Stars watalazimika kushinda ugenini leo, au kutoa sare ya kuanzia mabao 2-2 ili kusonga mbele, lakini vinginevyo wataishia hatua ya kwanza kabisa ya kuwania fainali za CHAN mwakani.
Nahodha Himid Mao alifunga bao la kusawazisha wiki iliyopita Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza
Kocha wa Amavubi, Antoine Hey amekuwa akimkatisha tamaa kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga kwamba sare ya 1-1 mjini Mwanza tayari ulikuwa ni ushindi kwa Rwanda na leo wanaingia Uwanja Kigali kukamilisha ratiba tu.
“Tumefanya mazoezi vizuri sana. Hatuna majeruhi na wachezaji wanaonekana kuelekeza fikra zao mno kwenye mchezo, kuliko ilivyokuwa kwenye mchezo wa kwanza. Kwa kweli, nafikiri tupo kwenye nafasi nzuri ya kumalizia kazi tuliyoianza Mwanza, hatupo chini ya presha,” amesema Hey.
“Mechi hii ni maalum mno kwetu na tunatakiwa kuianza vizuri kama tulivyofanya mechi ya kwanza tulipotangulia kufunga sisi, lakini tukaimalizia na walinzi wanane ili kulinda bao letu la ugenini, lakini sifikiri tutarudia mbinu zile zile mbele ya mashabiki wetu nyumbani,”alisema.
Kwa upande wake, kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga pia anajiamini kwamba watapata matokeo wanayoyahitaji leo mjini Kigali ili kusonga mbele.
Mayanga alisema wachezaji wake walicheza vizuri katika mchezo wa kwanza licha ya kulazimishwa sare, “Kuwaruhusu Amavubi kufunga bao la mapema lilikuwa kosa kubwa tulilofanya upande wetu. Tulicheza vizuri sana, tulitawala mchezo, tulikuwa na nafasi nyingi za kufunga ili kushinda mchezo, lakini tuliambulia sare tu, matokeo ambayo hatukuyatarajia kabisa. Lengo kubwa ni kuhakikisha tunarakebisha makosa Jumamosi,”alisema.
Katika mchezo wa kwanza, mchezaji mpya wa AS Kigali, Dominique Savio Nshuti aliifungia Rwanda bao la kuongoza dakika ya 18, kabla ya Nahodha wa Taifa Stars Himid Mao kuisawazishia timu yake kwa penalti dakika ya 35.
Mshindi wa jumla baina ya Rwanda na Tanzania atamenyana na mshindi kati ya Uganda au Sudan Kusini katika hatua ya mwisho ya mchujo mwezi ujao. Kila la heri Taifa Stars. Mungu ibariki timu yetu, wabariki wachezaji wetu. Mungu ibariki Tanzania yetu ing’are leo ugenini na kuwapa faraja wananchi wake. Amin.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2ukuEsB
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang SHUGHULI PEVU AMAVUBI NA TAIFA STARS NYAMIRAMBO LEO. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2017/07/shughuli-pevu-amavubi-na-taifa-stars.html. Terimakasih atas perhatiannya.