Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
KAMA ilivyotarajiwa, Simba SC imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Stand United ya Shinyanga jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Wekundu wa Msimbazi wanafikisha pointi 65 baada ya ushindi wa leo wakiwa wamecheza mechi 29, mbili zaidi ya mabingwa watetezi, Yanga SC wenye pointi 62, ambao wanaweza kurudi kileleni kwa mabao zaidi, wakiifunga Mbeya City kesho Uwanja wa Taifa.
Katika mchezo huo uliokuwa mkali na wa kusisimua, Stand United ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa nyota wake, Suleiman Kassim ‘Selembe’ aliyefunga sekunde ya 58 dakika ya kwanza.
Juma Luizio (kushoto) akimpira beki wa Stand United, Ibrahim Job (katikati) leo Uwanja wa Taifa
Mchezaji huyo wa zamani wa Azam FC ya Dar es Salaam na Coastal Union ya Tanga, alifunga bao hilo akitumia makosa ya kiungo anayechezeshwa beki ya kati kwa sasa kutokana na uhaba wa nafasi hizo, Mghana James Kotei.
Na ikawa rahidi kwa kiungo huyo, Selembe kufunga baada ya kipa Mghana, Daniel Agyei naye kuvutika kutoka langoni, hivyo Mzanzibari huyo akanyunyiza mpira nyavuni kiulaini.
Simba walifanikiwa kusawazisha bao hilo dakika ya 23 kupitia kwa mshambuliaji wake, Juma Luizio anayecheza kwa mkopo kutoka Zesco United ya Zambia, aliyefunga kwa kichwa akiunganisha krosi ya winga Shiza Kichuya.
Juma Luizio tena akawainua vitini mashabiki wa Simba kwa kufunga bao la pili na la ushindi dakika ya 35, kwa mara nyingine akimalizia kazi nzuri ya Kichuya.
Kipindi cha pili milango ilikuwa migumu kwa pande zote mbili na Simba ikafanikiwa kuvuna pointi tatu kwa ushindi wa 2-1 na kurejea kileleni.
Kikosi cha Simba SC; Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Juuko Murshid, James Kotei, Shiza Kichuya/Abdi Banda dk78, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo, Juma Luizio/Pastory Athanas dk61, Jonas Mkude na Mohammed ‘Mo’ Ibrahim/Mwinyi Kazimoto dk51.
Stand United; Frank Muwonge, Aaron Lulambo/Rajab Rashid dk81, Jacob Massawe, Miraj Maka, Revocatus Richard, Erick Mulilo, Adam Salamba, Kheri Khalifa/Sixtus Sabilo dk70, Frank Khamis, Ibrahim Job na Suleiman Kassim ‘Selembe’.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2r8zQwO
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms