Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KAMATI ya Mashindano ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imewafungiwa mechi tatu na kuwatoza faini ya Sh. 500,000 kila mmoja wachezaji Deus Kaseke wa Singida United na Shaban Dihile wa Green Warriors kwa makosa ya kinidhamu.
Katika kikao chake cha Februari 13, mwaka huu, ambacho pamoja na mambo mengine ilipitia taarifa za mchezo wa Azam Sports Federation Cup (ASFC) baina ya Green Warriors na Singida United, Kamati imewatia hatiani wawili hao kwa kosa la kutoingia uwanjani na timu zao na hawakuwepo wakati timu hizo zikipeana mikono Januari 31 Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam.
Deus Kaseke anaweza kuichezea tena Singida United michuano ya ASFC kama itafuzu fainali tu
Taarifa ya Kamati kwa vyombo vya Habari leo imesema kwamba adhabu hiyo ni kwa mujibu wa kanuni ya ASFC(1) ambayo inaelekeza kutumika kanuni ya ligi husika na hivyo kanuni iliyotumika ni 37(7d).
Katika hatua nyingine, mchezaji mwingine wa Singida United Kambale Salita amepelekwa kwenye kamati ya nidhamu ya TFF kwa kosa la kumpiga mchezaji wa timu pinzani kwenye mchezo huo.
Wakati huo huo: Kikao cha kawaida cha kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) kinakutana Jumamosi Februari 17,2018 kwenye Hoteli ya Sea Scape,Mbezi Beach,Dar Es Salam.
Kikao hicho cha kawaida kinachokutana kila baada ya miezi mitatu kitakuwa na ajenda kwa mujibu wa katiba ya TFF kupitia na kutathmini utendaji wa Shirikisho.
Kikao hicho cha kamati ya Utendaji kinatanguliwa na vikao vya kamati mbalimbali za TFF ambazo zimeanza kukutana kwa wiki mbili na wiki hii vikao vya kamati hizo vinaendelea.
Wajumbe wa Kikao cha kamati ya Utendaji wanaanza kuwasili kesho Ijumaa Februari 16, 2018 na watafikia kwenye Hoteli ya Sea Scape.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE http://ift.tt/2oaFbns
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang DEUS KASEKE, DIHILE WAFUNGIWA ASFC NA KUPIGWA FAINI KALI. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2018/02/deus-kaseke-dihile-wafungiwa-asfc-na.html. Terimakasih atas perhatiannya.