MABINGWA wa Kenya, Gor Mahia wamefuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho la Afrika licha ya kufungwa mabao 2-1 na wenyeji, Supersport United katika mchezo wa marudiano wa mchujo jana Uwanja wa Lucas Moripe mjini Pretoria, Afrika Kusini.
Gor Mahia walio chini ya kocha wa zamani wa Simba ya Tanzania, Dylan Kerr raia wa Uingereza wanasonga mbele kwa faida ya mabao ya ugenini kuhesabiwa mara mbili, kufuatia sare ya jumla ya 2-2 baada ya awali kushinda 1-0 mjini Machakos siku 10 zilizotanguli.
Katika mchezo wa jana, bao la kujifunga la Nahodha wa Gor, Harun Shakava liliipa bao la kwanza Supersport mwanzoni mwa kiopindi cha pili, kabla ya Francis Kahata kuisawazishia timu ya Kenya dakika chache baadaye.
Na Thabo Mnyamane akaifungia Supersport United bao la pili dakika ya 68, lakini Gor wakasimama imara kutoruhusu mabao zaidi.
Baada ya mchezo huo, kocha wa Gor, Kerr alisema; "Nimefarijika sana na nimefurahi kwa mafanikio ya umoja huu wa wachezaji. Tumefanya hivi kwa Gor Mahia, tumefanya hivi kwa soka ya Kenya,”.
Francis Kahata (kulia) baada ya kuisawazishia Gor Mahia jana dhidi ya Supersport United Uwanja wa Lucas Moripe
MATOKEO YOTE MECHI ZA MCHUJO WA KUINGIA HATUA YA MAKUNDI KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA
Jumanne Aprili 17, 2018
CS la Mancha (Kongo) 1-5 AS Vita (DRC) (0-1)
USM Alger (Algeria) 4-0 Plateau United (Nigeria) (1-2)
El Masry (Misir) 2-1 Mounana (Gabon) (1-1)
CR Belouizdad (Algeria) 0-0 ASEC Mimosas (Ivory Coast) (0-1)
Jumatano, Aprili 18, 2018
Raja Club Athletic (Morocco) 3-0 Zanaco (Zambia) (2-0)
CARA (Kongo) 1-0 (4-3pen) Saint George (Ethiopia) (0-1)
Akwa United (Nigeria) 3-1 El Hilal (Sudan) (0-2)
Supersport (Afrika Kusini) 2-1 Gor Mahia (Kenya) (0—1)
Hilal Obied (Sudan) 2-1 UD Songo (Msumbiji) (1-3)
Enyimba (Nigeria) 0-0 Bidvest (Afrika Kusini) (1-1)
Fosa Juniors (Madagascar) 2-1 Aduana (Ghana) (1-6)
Wolaitta Dicha (Ethiopia) 1-0 Yanga SC (Tanzania) (0-2)
RS Berkane (Morocco) vs Generation Foot (Senegal) (1-3)
Niefang (Equatorial Guinea) 2-1 Williamsville (Ivory Coast) (0-2)
Djoliba (Mali) vs MFM (Nigeria) (1-0)
Costa do Sol (Msumbiji) 2-0 Rayon Sports (Rwanda) (0-3)
TIMU ZOTE ZILIZOFUZU;
AS Vita (DRC), USM Alger (Algeria), El Masry (Misir), CARA (Kongo), El Hilal (Sudan), Gor Mahia (Kenya), UD Songo (Msumbiji), Enyimba (Nigeria), Aduana (Ghana), Yanga SC (Tanzania), RS Berkane (Morocco), Williamsville (Ivory Coast), Djoliba (Mali), Rayon Sports (Rwanda), Raja Club Athletic (Morocco)
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE https://ift.tt/2HPLc2J
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms