Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeitaka klabu ya Yanga SC kufanya Uchaguzi wa kuziba nafasi za viongozi wake waliojiuzulu ifikapo Januari 13 mwakani, 2019.
Mwenyekiti mpya wa Kamati ya Uchaguzi TFF, Malangwe Mchungahela amewaambia Waandishi wa Habari leo mjini Dar es Salaam kwamba Yanga inatakiwa kuanza mchakato wa uchaguzi wake ambao lazima ufanyike Januari 13, 2019.
Mchungahela amezitaja nafasi zitakazogombewa katika uchaguzi huo ni za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wanne wa Kamati ya Utendaji.
Na hiyo inafuatia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kuiagiza Yanga kuitisha uchaguzi wa kujaza nafasi za viongozi waliojiuzulu ili kuwa na safu imara ya uongozi.
Mwenyekiti mpya wa Kamati ya Uchaguzi TFF, Malangwe Mchungahela ameitaka Yanga kufanya uchaguzi wake Januari 13 mwakani
BMT ilisema katika taarifa yake kwa vyombo vya Habari wiki iliyopita kwamba, Yanga imebaki na Wajumbe sita kati ya 13 waliochaguliwa katika uchaguzi wa Juni 12, mwaka 2016 Dar es Salaam, hivyo inatakiwa kufanya uchaguzi wa kuziba nafasi zilizo wazi katika uongozi kwa mujibu wa katiba yao.
Tamko la BMT lilifuatia vikao vilivyohusisha Wazee, Wanachama, Viongozi na wadau mbalimbali wa klabu hiyo vilivyohudhuriwa hadi na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe.
BMT ilisema kwamba uchaguzi huo utasimamiwa na TFF kutokana na mapungufu ya Akidi katika Kamati ya Uchaguzi ya klabu hiyo.
Na kuhusu mkanganyiko wa kadi za uanachama, BMT imeagiza lifanyike zoezi la kusajili wanachama wenye kadi za zamani ili kurejesha umoja na mshikamano ndani ya klabu.
Yanga SC imebaki na Wajumbe sita tu baada ya viongozi wote wakuu kujiuzulu kwa wakati tofauti, akiwmeo Mwenyekiti, Yussuf Manji na Makamu wake, Clement Sanga.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE https://ift.tt/2QjsL9L
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms