Na Sada Salmin, DAR ES SALAAM
YANGA SC imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Biashara United ya Musoma mkoani Mara usiku wa leo Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
Ushindi huo unaifanya Yanga SC ifikishe pointi 41 baada ya kucheza mechi 15, sawa na Azam FC wenye pointi 39 ambao wanarejea nafasi ya pili, wakati mabingwa watetezi, Simba SC wenye pointi 27 za mechi 12 wanaendelea kushika nafasi ya tatu.
Haukuwa ushindi mwepesi kwa Yanga SC inayofundishwa na kocha Mwinyi Zahera kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), kwani kwa mara ya pili mfululizo ililazimika kutokea nyuma baada ya kutanguliwa na wapinzani.
Kama ilivyokuwa ikishinda 3-1 dhidi ya Tanzania Prisons mjini Mbeya kwenye mechi iliyopita – na leo Yanga walitanguliwa kwa bao la Abdulmajjid Mangalo dakika ya 38 aliyawazidi mbio mabeki wa timu hiyo baada ya kutanguliziwa mpira mrefu, Biashara wakitoka kuzuia shambulizi la wenyeji.
Baada ya bao hilo, Biashara wakaendelea kucheza kwa kujilinda vizuri na kuzuia mashambulizi mengi ya Yanga SC kiasi cha mashabiki wa wenyeji kuanza kukata tamaa.
Lakini kwa mara nyingine, Zahera akaonyesha weledi wake kwa mabadiliko yaliyokwenda kuiongezea kasi timu hadi kutokea nyuma tena na kushinda.
Zahera ambaye pia ni Kocha Msaidizi wa timu ya taifa ya DRC, aliwatoa viungo Feisal Salum ‘Fei Toto’, Mzimbabwe, Thabani Kamusoko na Raphael Daudi na kuwaingiza Mkongo mwenzake, Papy Kabamba Tshishimbi, Pius Buswita na mshambuliaji Mrundi, Amissi Tambwe.
Na ni Tambwe aliyempasia beki Abdallah Hajji Shaibu ‘Ninja’ kuifungia Yanga SC bao la kusawazisha dakika ya 70, kama Mkongo Heritier Makambo kufunga bao la pili dakika ya 80.
Makambo alifunga bao ambalo lingekuwa la tatu kama si refa kukataa akidai alimchezea rafu mchezaji wa Biashara kabla ya kufunga.
Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Ramadhani Kabwili, Paul Godfrey, Mwinyi Hajji Mngwali, Andrew Vincent ‘Dante’, Kelvin Yondan, Abdallah Shaibu ‘Ninja’, Feisal Salum/Pius Buswita dk67, Thabani Kamusoko/Amissi Tambwe dk56, Heritier Makambo, Raphael Daudi/Papy Kabamba Tshishimbi dk41 na Jaffar Mohammed.
Biashara United; Nourdine Balora, Godfrey Mapunda, Juma Mpakala, Abdulmajjid Mangalo, Sospeter Kasori, George Makang’a, Lameck Chamkaga, Frank Sekule, Lenny Kissu, Wilfred Kourouma na Lambele Jerome.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE https://ift.tt/2G82sD0
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms