Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KOCHA wa zamani wa Taifa Stars, Dk Mshindo Msolla atapambana na Elias Mwanjala pekee kuwania Uenyekiti wa klabu ya Yanga katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Mei 5, mwaka huu mjini Dar es Salaam.
Hiyo ni baada ya mpinzani wake mwingine, Lucas Mashauri aliyekuwa anapewa nafasi kubwa ya kushinda kuenguliwa kutokana na kutojitokeza kwenye usaili, kufuatia Dk. Jonas Benedict Tiboroha, Mbaraka Hussein Igangula na Erick Ninga waliochukua fomu awali nao kujitoa.
Taarifa ya Kamati ya Uchaguzi ya Yanga inayoshirikiana na Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imesema kwamba katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti wamepitishwa wagombea wawili pia.
Dk Mshindo Msolla atapambana na Elias Mwanjala pekee kuwania Uenyekiti wa Yanga Mei 5
Hao ni Katibu wa zamani wa TFF, Frederick Wilfred Mwakalebela na Mbunge wa jimbo Ileje (CCM) Mheshimiwa, Janet Zebedayo Mbena baada ya Samuel Lukumay na Thobias Lingalangala kuenguliwa kwa pingamizi, kufuatia Yono Kevela, Titus Eliakim Osoro na Salum Magege Chota kujitoa.
Taarifa hiyo iliyosainiwa na Wenyekiti wote wa Kamati za Uchaguzi, Mawakili Malangwe Mchungahela wa TFF na Sam Mapande wa Yanga imesema kwamba wagombea tisa tu wamepitishwa kuwania Ujumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo.
Hao ni Dominick Albinus, Saad Mohamed Khimji, Hassan Yahya Hussein, Shafiru Amour Makosa, Mhandsi Bahati Faison Mwaseba, Hamad Ali Islam, Mhandisi Leonard Marangu, Suma Mwaitenda na Haruna Hussein Batenga.   
Na hiyo ni baada ya wagombea wengine kujitoa, ama kuenguliwa kwa mapingamizi au kutokukidhi vigezo baada ya usaili jana wakiwemo Siza Augustino Lymo, Tobias Lingalangala, Samuel Lukumay na Hussein Nyika.
Wengine waliojiuzulu katika uongozi wa Yanga uliongia madarakani Juni 11 mwaka ni aliyekuwa Mwenyekiti Yussuf Manji, Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na wajumbe wanne, Omary Said Amir, Salum Mkemi, Ayoub Nyenzi na Hashim Abdallah. 
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE http://bit.ly/2IqEZ03
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms