Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amelitaka Baraza la Michezo (BMT) kumpa majibu ya malalamiko ya maamuzi katika ligi mbalimbali nchini ndani ya siku tatu kuanzia kesho Februari 6, 2020.
Waziri Mwakyembe amechukua hatua hiyo kufuatia kuwepo kwa mfululizo wa matukio ya uonevu baina ya vilabu hususani maamuzi ya viwanjani hasa katika Ligi Kuu.
“Wizara imeendelea kupokea tuhuma mbalimbali/uonevu katika mashindano ya ligi mbalimbali za mpira wa miguu yanayoendelea nchini, lakini wadau hawaoni hatua zikichukuliwa mara moja na kupatiwa mrejesho,” imesema taarifa ya Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Eleuteri Mangi leo.
Tamko la Waziri Mwakyembe linakuja wakati tayari Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ameitaka Kamati ya Waamuzi kukutana na Bodi ya Ligi ili kutathmini mwenendo wa uchezeshaji wa Waamuzi wa Ligi Kuu.
Rais Karia amesema kwamba katika kikao hicho watakuwepo baadhi ya Maafisa wa TFF kutoka Idara ya Mashindano.
Rais Karia ametaka kikao hicho baina ya pande hizo tatu kitazame kwa kina kuhusu mwenendo wa uchezeshaji wa marefa ili kuondoa malalamiko katika eneo hilo ambalo ni muhimu katika maendeleo ya mpira wa miguu nchini.
Na hayo yanafuatia mfululizo wa matukio ya marefa ya kutoa maamuzi mabovo kwenye Ligi Kuu, zaidi yakionekana kuwanufaisha mabingwa watetezi, Simba SC.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE https://ift.tt/2Sla08d
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms