Na Alfred Lucas, CAIRO
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania maarufu kwa jina la Taifa Stars, inatarajiwa kurejea Dar es Salaam leo kutoka Misri ambako iliweka iliweka kambi ya wiki kujiandaa na mchezo wa Kundi L kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2019 dhidi ya Lesotho Juni 10, Uwanja.
Taifa Stars wanatarajiwa kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Saa 6.30 mchana wa leo.
Timu hiyo iliyosafiri kwa ndege wa Ethiopia, ilikuwa jijini Alexandria - Kaskazini kabisa mwa nchi ya Misri ambako ilipiga kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Lesotho unaotarajiwa kufanyika Jumamosi Juni 10, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Akizungumza mara baada ya mazoezi ya jana asubuhi, Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Salum Mayanga amesema kwamba kimsingi amefanikiwa katika kile alichopangilia kukifanya akiwa Misri.
“Kwanza kabisa niweze kumshukuru Mungu. Tulisafiri salama na kufanya mazoezi kwa siku saba hapa Misri. Na leo jioni tunanza safari ya kuelekea Cairo kwa ajili ya safari ya kurudi nyumbani. Naam, kambi ilianza tarehe 23 mwezi uliopita pale Dar es Salaam na tukaja kuendelea huku Misri.
“Naweza kusema kuwa nimefanikiwa au tumefanikiwa. Kambi ni nzuri, mazingira ya kambi ni mazuri na tulifika mahali ambako hakuna mtu anayeweza kufanya movement (mizunguko) zozote za kutoka au kuingia kirahisi kwa sababu tulikuwa kwenye kambi ya Hoteli ya Nyota Tano, lakini ni Jeshi.
“Mazoezi ya kawaida ya kiufundi napo tumefanya vema kwa maana wana vitu vyote tunavyohitaji vilipatikana hasa kufanya mazoezi usiku kwa sababu mchezo wetu utakuwa usiku. Nawaomba tu Watanzania waje kuiunga mkono timu yao,” amesema Mayanga.
Naye, Nahodha Msaidizi wa timu hiyo, Himid Mao Mkami, amesema kwamba kambi ilikuwa nzuri yenye mafanikio ambayo matunda yake yatakuja kuonekana katika michezo mbalimbali ya kimataifa ukiwamo wa Jumamosi dhidi ya Lesotho.
Mchezo huo dhidi ya Lesotho umepangwa kuanza Saa 2:00 usiku Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuwania nafasi muhimu ya kucheza fainali za AFCON za mwaka 2019 zitakazofanyika Cameroon.
Mbali ya Lesotho na Tanzania, mataifa mengine katika Kundi ‘L’ ni Uganda na Cape Verde ambao pia wikiendi ya Juni 9, 10 na 11, mwaka huu watakuwa katika mchezo wa kwanza pia kuwania nafasi hiyo.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2rK72MU
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang STARS YAREJEA LEO, MECHI NA LESOTHO KUCHEZWA USIKU DAR. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2017/06/stars-yarejea-leo-mechi-na-lesotho.html. Terimakasih atas perhatiannya.