KOCHA Julen Lopetegui ameondoka Urusi kufuatia kufukuzwa timu ya Hispania siku mbili kabla ya fainali za Kombe la Dunia.
Lopetegui alifukuzwa jana Hispania kufuatia kutangazwa kuwa kocha mpya wa Real Madrid akiwa maandalizi ya mwisho ya Kombe la Dunia.
Na usiku wa jana, kocha huyo mwenye umri wa miaka 51 alipigwa picha akipakia mizigo yake kwa safari ya Uwanja wa Ndege wa Krasnodar kurejea Hispania.
Taarifa zinasema mchana wa leo Alhamisi, Lopetegui angeweza kutambulishwa kama kocha mkuu wa Madrid kwenye uwanja wa timu hiyo wa Santiago Bernabeu.
Akizungumza kabla ya kuondoka jijini Krasnodar, huko Urusi, Lopetegui amesema. "Imeniuma sana, lakini nawatakia Hispania mafanikio mema katika Kombe la Dunia ikiwezekana kutwaa ubingwa," amesema Lopetegui akiwa katika uso unaomaanisha kile asemacho. "
Miongoni mwa changamoto zinazomkabiri Lopetegui kwa sasa katika kibarua chake kipya ni majaliwa ya nyota kadhaa wa Madrid ambao baadhi yao ni Cristiano Ronaldo, Odriozola, Alisson, na Gareth Bale.
Tayari kocha mpya wa Hispania, Fernando Hierro ameanza kazi na kusema ana matumaini ya kufanya vizuri huku akisisitiza kutofanya mabadiliko yoyote yale kikosini.
Hierro ambaye ni nyota wa zamani wa Klabu ya Real Madrid amepewa kazi ya kuinoa Hispania baada ya Kocha Julen Lopetegui kutimuliwa katika nafasi hiyo kutokana na kitendo chake cha kutangazwa kuwa kocha mpya wa Madrid.
Hispania ipo Kundi B katika fainali za Kombe la Dunia zinazoanza leo saa 12:00 jioni na itacheza mechi yake ya kwanza Ijumaa wiki hii dhidi ya Ureno.
“Ni wakati wangu mzuri wa kuwajibika na kuwathibitishia walionipa majukumu, kwa mazingira yalivyo sitafanya mabadiliko yoyote yale na niwatake mashabiki wetu kutoamisha matarajio yao, tutafanya vizuri,” amesema Hierro.
Jumanne wiki hii Madrid ilimtangaza Lopetegui kuwa kocha wake mpya akichukua mikoba ya Zinedine Zidane huku akielezwa kuanza kazi baada ya Kombe la Dunia, lakini Shirikisho la Soka la Hispania kupitia kwa rais wake, Luis Rubiales liliamua kumfuta kazi kwani hakuwa amewaeleza lolote kuhusu mpango wake huo wa kwenda Madrid.
Licha ya baadhi ya wachezaji wakongwe wa kikosi cha Hispania kushauri kocha huyo kutotimuliwa, Rubiales alimtimua na kumtangaza Hierro kuwa kocha moya kutoka katika nafasi ya mkurugenzi wa ufundi.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE https://ift.tt/2sWbdHk
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang LOPETEGUI AONDOKA URUSI KWA AIBU, ATUA MADRID KIFALME. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2018/06/lopetegui-aondoka-urusi-kwa-aibu-atua.html. Terimakasih atas perhatiannya.