Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
SIMBA SC imetamba kwamba ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara upo kwenye njia yao baada ya kufanikiwa kuvuna pointi nne kwa wapinzani wakuu, Azam na Yanga.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba, Hajji Sunday Manara alisema jana katika mazungumzo na BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE kwamba sasa timu yao imekaa vizuri katika mbio za ubingwa dhidi ya Azam na Yanga.
“Kama unataka ubingwa, lazima uwashinde wapinzani wako wakuu na kushinda mechi nyingine zote. Sisi tumefanikiwa kuvuna pointi nne kwa wapinzani wetu, baada ya kutoa sare na Yanga na kuwafunga Azam, sasa maana yake ubingwa upo kwenye njia yetu zaidi,”alisema.
Aidha, Manara alisema kwamba Simba SC inaendelea vizuri na maandalizi yake ya mchezo wake wa kesho wa Ligi Kuu dhidi ya Toto Africans ya Mwanza.
Simba SC watawakaribisha Toto kesho Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam katika mfululizo wakitoka kushinda 1-0 dhidi ya timu nyingine ya Mwanza, Mbao FC Alhamisi.
Ushindi wa juzi ulikuwa wa mbinde, kwani timu ya kocha Joseph Marius Omog ililazimika kusubiri hadi dakika ya 87 wakati kiungo Muzamil Yassin aliyesajiliwa msimu huu kutoka Mtibwa Sugar alipofunga akimalizia krosi ya mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Frederick Blagnon.
Simba SC ndiyo inaongoza Ligi Kuu kwa pointi zake 26 baada ya kucheza 10 ikishinda nane na kutoa sare mbili – hivyo kuendelea kuwazidi kwa pointi sita Stand United walio nafasi ya pili, wakati mabingwa watetezi, Yanga wana pointi 18 za mechi tisa.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2et9al7
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang SIMBA SC: UBINGWA UPO TUNAKOPITA SISI. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2016/10/simba-sc-ubingwa-upo-tunakopita-sisi.html. Terimakasih atas perhatiannya.