Na Mwandishi Wetu, MACHAKOS
MSHAMBULIAJI wa Tanzania Bara, Mbaraka Yusuph hataweza kucheza mechi ijayo ya Kundi A Kombe la Challenge dhidi ya Zanzibar Desemba 7, mwaka huu baada ya jana kushindwa kufanya mazoezi kutokana na maumivu ya misuli.
Hayo yamethibitishwa na kocha Mkuu wa Kilimanjaro Stars, Ammy Conrad Ninje alipozungumza na Waandishi wa Habari nchini Kenya jana ambako michuano ya Challenge inafanyika mwaka huu.
Mbarak Yusuph ndiye mchezaji pekee ambaye hakufanya mazoezi jana baada ya kuumia misuli kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi A juzi dhidi ya Libya timu zikitoka sare ya 0-0.
Mbaraka Yusuph aliumia katika mchezo dhidi ya Libya juzi Uwanja wa Kenyatta mjini Machakos
Baada ya sare ya 0-0 na Libya juzi, Kilimanjaro Stars itarudi uwanjani keshokutwa kumenyana na ndugu zake, Zanzibar kabla ya Desemba 9 kucheza na Rwanda na Desemba 11 kukamilisha mechi zake za Kundi A kwa kumenyana na wenyeji, Kenya.
Ninje amepanga kutumia mazoezi ya leo kufanyia kazi mapungufu yaliyoonekana kwenye mchezo dhidi ya Libya ili timu ipate matokeo mazuri kwenye mechi zijazo.
Ninje amesema katika mchezo huo wa kwanza walicheza katika kiwango cha kuridhisha na kikubwa anataka kuangalia namna ya kufanyia kazi upungufu ikiwa ni pamoja na pale timu inapopoteza mpira.
Anasema kwenye mchezo dhidi ya Libya timu ilicheza kuanzia nyuma kupitia sehemu ya kiungo na kuunganisha sehemu ya ushambuliaji – jambo ambalo limemfurahisha kwa namna timu ilivyotengeneza nafasi.
Akizungumzia mchezo unaofuata dhidi ya Zanzibar Heroes, Ninje amesema ni mchezo mgumu kama ambavyo historia inaonesha wakati timu hizo mbili zinapokutana.
“Lakini kuanzia mazoezi ya kesho nitaiandaa timu kupata ushindi na nimepanga kwenda kuitazama Zanzibar itakapocheza mchezo wake wa kesho dhidi ya Rwanda,” amesema.
Amesema ataiangalia Zanzibar Heroes kiufundi ili kubaini upungufu wao ili naye ajue namna atakavyoweza kutumia nafasi hizo kwenye mchezo unaofuata.
“Ni fahari kwa timu zetu hizi mbili kila mmoja kupambana kupata pointi bahati nzuri wao wanacheza kesho kwa hiyo mchezo wao nitautumia kutazama mapungufu (upungufu wao) yao yatakayoweza kutusaidia,’’ alisema Ninje.
Kilimanjaro Stars ipo kundi A pamoja na timu za Zanzibar, Libya, Rwanda na wenyeji Kenya.
Kenya wana pointi tatu baada ya kuifunga Rwanda mabao 2-0 wakati Kilimanjaro Stars na Libya wana pointi 1 kila mmoja baada ya kutoka sare ya bila kufungana kwenye mchezo wao wa kwanza wakati Zanzibar na Rwanda wenyewe hawana pointi huku Zanzibar ikiwa haijashuka dimbani katika kundi hilo.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE http://ift.tt/2AMDPrD
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang STARS KUMKOSA MBARAKA YUSUPH MECHI NA ZANZIBAR KESHOKUTWA. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2017/12/stars-kumkosa-mbaraka-yusuph-mechi-na.html. Terimakasih atas perhatiannya.