Na Mwandishi Wetu, MACHAKOS
BEKI wa kati wa Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’, Kelvin Yondani ataukosa mchezo wa Kundi A Kombe la CECAFA Challenge kesho dhidi ya Rwanda Uwanja wa Kenyatta, Machakos nchini Kenya.
Yondani amepewa mapumziko ya siku tatu baada ya kuumia kifundo cha mguu kwenye mchezo wa jana dhidi ya Zanzibar, Bara ikichapwa 2-1.
Hivyo atakosa mchezo huo wa kesho ukiwa ni miongoni mwa mechi mechi za michuano ya kuwania Kombe la Afrika Mashariki maarufu kama Cecafa Senior Challenge inayofanyika hapa Kenya.
Jopo la Madaktari wa Kilimanjaro Stars linaloundwa na Dk. Richard Yomba na Dk Gilbert Kigadye limethibitisha kuwa majeraha aliyoyapata Yondani sio makubwa na yanahitaji apumzike kwa saa 72 ambazo ni sawa na siku tatu.
Kelvin Yondani ataukosa mchezo dhidi ya Rwanda kesho Uwanja wa Kenyatta, Machakos nchini Kenya
Vipimo vilivyochukuliwa vinaonesha kuwa hakuna mfupa wowote ulioathirika zaidi ya kupata mshtuko kiasi kwa hiyo wamempa siku tatu za mapumziko wakiendelea kumtazama maendeleo yake kwa ukaribu.
Kwa upande wa Mbaraka Yusuph ambaye alipata majeraha ya misuli kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Libya, amepona na anatarajia kuingia kwenye program ya utimamu wa mwili.
Hata hivyo Mbaraka hataweza kucheza kwenye mchezo wa kesho dhidi ya Rwanda.
Wakati huo huo, leo kikosi cha Kilimanjaro Stars kimefanya mazoezi kwenye Uwanja wa Machakos Academy licha ya mvua zinazoendelea kunyesha hapa County ya Machakos.
Kilimanjaro inajiandaa na mchezo wa kesho dhidi ya Rwanda utakaochezwa saa 8 mchana kwenye Uwanja wa Kenyatta, Machakos.
Mchezo huo wa kundi A una umuhimu mkubwa kwa Kilimanjaro Stars katika harakati zake za kuitafuta tiketi ya kucheza hatua ya nusu fainali.
Kilimanjaro Stars ina pointi moja mpaka sasa baada ya kutoka sare na Libya kwenye mchezo wa kwanza kabla ya kufungwa na Zanzibar kwenye mchezo wake wa pili.
Kundi A linaongozwa na Zanzibar wenye pointi sita (6) wakifuatiwa na Uganda wenye pointi (4) wakati Libya yenyewe ina pointi (3) ikikamata nafasi ya tatu ikifuatiwa na Kilimanjaro Stars na Rwanda wenye pointi (1) kila mmoja.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE http://ift.tt/2y83tS4
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms