MFADHILI na Mdhamini wa klabu ya Yanga, Bilionea Ghalin Said Mohamed amemtembelea kumjulia hali na kumpa pole kiungo Muivory Coast, Peodoh Pacome Zouzoua aliyeumia jana kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara, dhidi ya wenyeji, JKT Tanzania Uwanja wa Meja Jenerali Charles Isamuhyo, Mbweni, Dar es Salaam.
Pamoja na Ghalib, viongozi wa Yanga wakiongozwa na Rais, Hersi Ally Said, wachezaji wenzake, na wa klabu nyingine akiwemo Kocha Mkuu wa Azam FC, Jean-Florent Ikwange Ibengé raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) pia wamemtembelea mchezaji huyo kumpa pole na kuomuombea apone mapema.
Pacome anaweza kuwa nje ya Uwanja kwa muda wiki sizizopungua sita kuangalia hali yake baada ya kuumia goti jana kwenye mchezo huo ambao Yanga SC ilishinda mabao 3-0 na kutwaa ubingw awa ligi hiyo kwa mara ya tano mfululizo.
Hiyo ni baada ya Pacome kufanyiwa upasuaji usiku wa jana kwenye hospitali ya Aga Khan kufuatia kuumia goti alipogongana na kiungo wa JKT Tanzania, Hassan Wahabi mwishoni mwa kipindi cha kwanza – na kukimbizwa hospitali moja kwa moja.
Afisa habari wa Yanga, Ally Shaaban Kamwe amesema baada ya wiki hizo atafanyia uchunguzi mwingine ili kujua tena mustakabali wa maumivu yake.
“Siku ya jana, Pacome alipata jeraha kubwa lililohitaji matibabu ya haraka. Baada ya tathmini iliyofanywa na jopo la madaktari wa Klabu kwa kushirikiana na madaktari wa Hospitali ya Agha Khan, ilikubaliwa afanyiwe upasuaji,” amesema Kamwe na kuongeza.
“Majira ya saa nane usiku, upasuaji huo ulifanyika na kukamilika kwa mafanikio. Kwa sasa, Pacome atakuwa chini ya uangalizi wa karibu kwa kipindi cha wiki sita, ambapo baada ya hapo tathmini nyingine itafanyika ili kubaini muda atakaohitaji kabla ya kurejea uwanjani,”.
Uongozi wa JKT Tanzania na mchezaji Hassan Wahabi wamemtembelea Pacome hospitalini kumpa pole baada ya tukio la jana katika mchezo wa kuhitimisha msimu wa Ligi Kuu.
from BIN ZUBEIRY SPORTS — ONLINE https://ift.tt/Wkpshdf
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms