Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
SIMBA SC imeanza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa kishindo kufuatia ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Ndanda FC ya Mtwara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Japokuwa hakufunga hata bao moja, lakini beki wa kulia Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ ndiye anastahili sifa zaidi kwa ushindi mnono wa Simba leo, kutokana na kuseti mabao yote.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Emmanuel Mwandembwa wa Arusha, hadi mapumziko timu hizo zilikuwa zimefungana bao 1-1.
Simba SC walitangulia kwa bao la mshambuliaji kutoka Burundi, Laaudit Mavugo dakika ya 20 aliyemalizia mpira wa adhabu wa Tshabalala.
Mshambuliaji anayeinukia vizuri nchini, Omary Mponda akaisawazishia Ndanda FC dakika ya 37 kwa kichwa akimalizia krosi ya Nahodha Kiggi Makassy.
Mabadiliko yaliyofanywa na kocha Mcameroon wa Simba, Joseph Marius Omog kipindi cha pili akiwatoa Jamal Mnyate na Ibrahim Hajib na kuwaingiza Mwinyi Kazimoto na Frederick Blagnon yaliiongezea uhai Simba na kuvuna mabao zaidi.
Mshambuliaji kutoka Ivory Coast, Blagnon alianza kuifungia Simba SC bao la pili dakika ya 73 kwa kichwa akimalizia kona ya Tshabalala.
Nyota wa mchezo wa leo, Tshabalala akaseti bao la tatu baada ya kupiga kona iliyotemwa na kipa Jackson Chove na winga Shizza Ramadhani Kichuya akasukumia nyavuni kuipa Simba SC ushindi wa 3-1.
Kwa ujumla Simba SC imecheza leo na ilistahili ushindi huo, wakati Ndanda walionyesha upinzani kwa wenyeji kipindi cha kwanza pekee.
Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Vincent Angban, Hamad Juma, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Novaty Lufunga, Method Mwanjali, Jonas Mkude, Shizza Kichuya/Mohamed Ibrahim dk84, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo, Ibrahim Hajib/Frederick Blagnon dk62 na Jamal Mnyate/Mwinyi Kazimoto dk69.
Ndanda FC; Jackson Chove, Azizi Sibo/Bakari Mtama dk65, Paul Ngalema, Kiggi Makasi, Hemed Khoja, Salvatory Ntebe, Forahim Isihaka, Bryson Raphael, Salum Telela, Omary Mponda na Shija Mkina/Nassor kapama dk65.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2b7DvCN
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms