Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KOCHA maarufu wa zamani nchini, Mohammed Hassan Msomali amefariki dunia mchana wa leo mjini Morogoro.
Taarifa iliyothibitishwa na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ni kwamba Msomali aliyewahi kuchezea timu mbalimbali Morogoro, ikiwemo Mseto amefariki dunia leo.
“Ni kweli Msomali amefariki dunia, na mimi nimepata taarifa hizo leo. Tumezipokea kwa masikitiko makubwa taarifa hizi, soka ya Tanzania imempoteza gwiji na mtu muhimu sana,”alisema Malinzi.
Buriani Mohammed Hassan Msomali, soka ya Tanzania imempoteza gwiji na mtu muhimu
Msomali alianza kuwika kama mchezaji na alikuwemo katika kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kilichoshiriki Michezo ya Afrika mjini Lagos nchini Nigeria mwaka 1973 pamoja na magwiji wengine kama Maulid Dilunga, Omary Mahadhi ambao wote tayari marehemu pia na Abdallah KIbadeni.
Kocha huyo wa mabingwa wa Tanzania Bara mwaka 1975, Mseto ya Morogoro – aliwahi pia kufundisha timu za taifa za Bara na Muungano, Taifa Stars, akisaidiwa na Mzee Kategile, baba wa winga wa zamani wa Simba, Alfred Kategile kuanzia mwaka 1980 hadi 1983.
Msomali atakumbukwa zaidi Morogoro kwa kuibua vipaji vya wachezaji wengi kitaifa, akiwemo Zamoyoni Mogella, aliyemuita timu ya Bara mwaka 1981, licha ya kuonekana mdogo kwa sababu ya umbo lake, lakini akaibuka mfungaji bora wa mashindano.
Pamoja na kucheza na kufundisha, Msomali pia amewahi kushika nyadhifa mbalimbali, ikiwemo Ujumbe wa Kamati ya Nidhamu ya TFF miaka minne iliyopita. Kabla ya kifo chake, Msomali alikuwa mmoja wa wakufunzi wa ukocha nchini.
Buriani. Gwiji wa soka Morogoro na Tanzania, Mohamed Hassan Msomali. Hakika sisi sote ni haki yake kwa Allah tutarejea. Allah akupe kauli thabiti inshaallah. Pumzika kwa amani Msomali.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2cwXYTv
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang KOCHA MSOMALI AFARIKI DUNIA MOROGORO. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2016/09/kocha-msomali-afariki-dunia-morogoro.html. Terimakasih atas perhatiannya.