Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania, Mrisho Khalfan Ngassa anatarajiwa kurejea nyumbani kwa matatizo ya kifamilia.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE leo kwa simu kutoka Muscat, Oman, Ngassa alisema kwamba amepata matatizo ya kifamilia na atakuja nchini kwa muda baada ya kuruhusiwan na klabu yake Fanja.
“Nimeruhusiwa, nitakuwa huko siku mbili hizo,”alisema Ngassa ambaye amejiunga na Fanja Septemba mwaka huu na kuongeza; “Kuna mambo mengine yanatokea katika familia hakuna namna nyingine zaidi ya kuacha kazi na kwenda kushiriki,”.
Mrisho Ngassa (kulia) anatarajiwa kurejea nyumbani kwa matatizo ya kifamilia
Aidha, Ngassa alisema wakati anajiandaa kwa safari ya kurudi nyumbani kwa matatizo ya kifamilia, aliumia mazoezini hivyo atakapaokuwa Tanzania itabidi atibiwe kabisa ili arejee Oman akiwa fiti.
“Ningesema nitibiwe kwanza kule ndiyo nirudi nyumbani, ningechelewa, kwa hiyo nimewaomba wakati nikiwa huku nitibiwe kabisa ndiyo nirudi. Kwa hiyo ninaweza kukaa kidogo kama wiki hivi,”alisema.
Tayari Ngassa amefunga bao moja katika mchezo wa Ligi Kuu ya Oman, Fanja ikilazimishwa sare ya 1-1 na Al-Nahda Uwanja wa Seeb, Muscat.
Ngassa alijiunga na Fanja mwezi uliopita kwa mkataba wa miaka miwili akitokea ya Free State Stars ya Afrika Kusini, baada ya kuomba mwenyewe kuvunja Mkataba.
Ngassa alijiunga na Free State Stars Mei mwaka jana akisajiliwa na kocha Mmalawi, Kinnah Phiri kwa mkataba wa miaka minne.
Hata hivyo, kocha aliyemsajili baba huyo wa Farida (9) na Faria (7) alifukuzwa baada ya miezi miwili tu na sasa tayari yuko Mbeya City ya Tanzania.
Katika kipindi cha mwaka mmoja wa kuwa Free State, Ngassa alifanya kazi na makocha wanne akiwemo huyu wa sasa, Mfaransa Denis Lavagne aliyeanza kazi Juni mwaka huu.
Wengine ni Mjerumani Ernst Middendorp aliyefanya kazi kati ya Septemba na Desemba 2015, Mtaliano Giovanni Solinas aliyefanya kazi kati ya Desemba na Mei 2016.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2fjxRBN
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang NGASSA AREJEA NYUMBANI KWA MATATIZO YA KIFAMILIA. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2016/11/ngassa-arejea-nyumbani-kwa-matatizo-ya.html. Terimakasih atas perhatiannya.