Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
HATIMAYE wachezaji wa Yanga wamesitisha mgomo wao uliodumu kwa siku mbili, baada ya kuahidiwa kulipwa mishahara yao ya Novemba kabla ya ijumaa.
Mmoja wa wachezaji wa Yanga ameiambia Bin Zubeiry Sports – Online usiku huu kwamba wamemaliza mgomo wao baada ya kuahidiwa kwamba wataingiziwa mishahara kabla ya mechi ijayo, Ijumaa dhidi ya African Lyon.
“Tumemalizana, wametuambia kila kitu wataweka sawa na kabla ya mechi (Ijumaa) kila mtu atakuwa amekwishaingiziwa mshahara wake,”amesema mchezaji huyo ambaye hakutaka kutajwa.
wachezaji wa Yanga wamesitisha mgomo wao uliodumu kwa siku mbili, baada ya kuahidiwa kulipwa mishahara yao ya Novemba kabla ya Ijumaa
Wachezaji wa Yanga kwa siku ya pili leo wameendelea na mgomo wa kufanya mazoezi wakishinikiza walipwe mishahara yao ya Novemba.
Ni wachezaji wawili tu walioonekana Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam asubuhi ya leo, kipa Ally Mustafa ‘Barthez’ na beki Oscar Joshua.
Zaidi ya hapo walitokea makocha tu, George Lwandamina na Wasaidizi wake, Noel Mwandila Mzambia mwenzake na wazalendo, Juma Mwambusi, kocha wa makipa Juma Pondamali, Meneja Hafidh Saleh, Daktari Edward Bavu, Mchua Misuli Jacob Onyango na Mtunza Vifaa Mohammed Omar ‘Mpogolo’.
Kaimu Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit alifika Uwanja wa Uhuru na kukutana na hali hiyo ya kushangaza na akaenda kuzungumza na Lwandamina baadaye Mwambusi na Hafidh.
Baada ya hapo wote wakaondoka na leo asubuhi mazoezi hayakufanyika Yanga.
Mgomo huo ulianza jana ghafla Uwanja wa Uhuru, wachezaji wakiwa wamekwishavaa, wakagoma kuingia mazoezini.
Mapema leo, uongozi wa Yanga ulikanusha kuwapo kwa madai ya mishahara ya Novemba na kudai kwamba wachezaji wanagoma wakitaka walipwe mapema mishahara ya mwezi huu, Desemba.
“Kinacholeta matatizo hapa ni kubadilika kwa mfumo wa ulipaji, yaani badala mwishoni mwa mwezi, sasa tunalipa mwanzoni mwa mwezi. Sasa wachezaji wanataka mishahara ya Desemba walipwe mapema kwa sababu ya hizi sikukuu,”alisema Baraka akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online leo.
from BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE http://ift.tt/2hRCTJ0
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms