Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
TIMU ya JKT Ruvu inayoshiriki Ligi Daraja La Kwanza Tanzania Bara Kundi A msimu huu, sasa itajulikana kwa jina la JKT Tanzania SC.
Taarifa ya Msemaji wa timu, Afisa Mteule Daraja la Pili, Costantine Masanja, imesema kwamba JKT Tanzania ndiyo imepitishwa kuwa timu pekee inayomililikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa itakayobaki kwenye usajili wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Hiyo ni kufuatia TFF kuamua kutilia mkazo agizo la Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) juu ya mmiliki mmoja kutokuwa na timu zaidi ya moja katika ligi za nchi na Masanja amesema maskani ya JKT Tanzania yataendelea kuwa makao makuu ya jeshi hilo, Mlalakuwa.
“Mababadiliko haya yamekuja baada baada ya kupata maelekezo kutoka bodi ya ligi kwa taasisi kumiliki timu moja, taratibu zote zimefuatwa katika kutekeleza agizo hili, uongozi wa JKT Ruvu unatoa shukrani za dhati kwa Bodi Ya Ligi na TFF kwa ushirikiano mkubwa walioutoa kupitia mamlaka/idara zake wakati wa mchakato mzima kuhusu suala hili muhimu kwa ustawi wa taifa letu kupitia mpira wa miguu,”amesema.
Aidha, Masanja amesema Mwenyekiti wa JKT Ruvu, Luteni Kanali Hassan Mabena alikwishatolea ufafanuzi wa kina suala hilo kupitia baadhi ya vyombo vya habari.
JKT Tanzania kwa sasa ipo kambini na inaendelelea na mazoezi katika Uwanja wa Meja Jenerali Michael Isamuhyo, Mbweni JKT, chini ya kocha wake Mkuu, Bakari Shime, tayari kwa mchezo wake na Mvuvumwa FC Januari 13 Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Kocha Shime amedhamiria kuhakikisha timu yake inashinda michezo yote iliyobaki ili kutimiza malengo waliyojiwekea ya kurejea Ligi Kuu.
Pamoja na kushiriki Ligi Daraja la Kwanza, JKT Tanzania pia ipo katika hatua ya 32 Bora ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) na imepangwa kucheza na Polisi Dar es Salaam.
Historia ya JKT Tanzania inaanzia mwaka 1970 katika kambi ya JKT Mgulani mjini Dar es Salaam ilipoanzishwa kwa jina la JKT Kabambe, kabla ya mwaka 1973 kuhamishiwa katika kikosi cha Ruvu JKT mkoani Pwani na mwaka 1975 ikabadilishwa jina na kuitwa JKT Ruvu.
Mwaka 1999 timu hiyo ilihamishiwa makao makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa, Mlalakuwa mjini Dar es Salaam ingawa iliendelea kujulikana kama JKT Ruvuy hadi Desemba 12, mwaka jana ilipobadilishwa tena jina na kuwa JKT Tanzania.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE http://ift.tt/2F2HtwQ
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang JKT RUVU YABADILISHWA JINA TENA, SASA YAITWA JKT TANZANIA. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2018/01/jkt-ruvu-yabadilishwa-jina-tena-sasa.html. Terimakasih atas perhatiannya.