Na Mwandishi Wetu, OMDURAN
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Thomas Emmanuel Ulimwengu usiku wa jana ameifungia bao la pili El HIlal ikitoka sare ya 2-2 na Songo ya Msumbiji katika mchezo wa Kundi B Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Al-Hilal mjini Omdurman.
Ulimwengu alifunga bao hilo dakika ya 36 akimalizia pasi ya Mohamed Bashir, aliyefunga bao la kwanza dakika ya pili tu ya mchezo kwa pasi ya Sharaf Eldin Ali.
Dakika mbili kabla ya mapumziko, Songo ikafanikiwa kupata bao la kufutia machozi lililofungwa na kiungo Mmalawi, Frank Banda dakika ya 43 akimalizia pasi ya beki, Pascoal Amorim kabla ya mshambuliaji mkongwe Helder Pelembe kuisawazishia timu hiyo dakika ya 87.
Huu unakuwa ushindi wa kwanza kwa Hilal baada ya sare moja na kufungwa mechi moja kati ya mbili za awali na sasa inafikisha pointi nne ikifufua matumaini ya kwenda Nusu Fainali.
Ulimwengu amejiunga na El Hilal mwishoni mwa mwezi Mei baada ya kuachana na AFC Eskilstuna ya Sweden ambayo alishindwa kuitumikia vyema kutokana na kuandamwa na maumivu ya goti yaliyomlazimu kufanyiwa upasuaji katika hospitali ya Taasisi ya Sayansi ya Michezo mjini Cape Town, Afrika Kusini mwaka jana na kupitia kipindi kirefu cha mazoezi ya kujiweka fiti.
Ulimwengu alikwenda kwa watalaamu nchini Italia kufanyishwa mazoezi maalum ya kumuweka fiti haraka arejee uwanjani, ambayo hakika yamemsaidia hadi kuanza vyema na vigogo wa Sudan.
Maumivu ya goti yalikuwa yakimsakama Ulimwengu tangu alipojiunga na Eskilstuna Januari mwaka jana akitokea Tout Puissant Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kiasi cha kushindwa kucheza.
Ulimwengu aliyezaliwa Juni 14, mwaka 1993 aliibukia katika taasisi ya soka Tanzania (TSA) mwaka 2008, kabla ya mwaka 2009 kwenda kuanza kukomazwa Ligi Kuu katika klabu ya Moro United alikokuwa akicheza kwa mkopo hadi mwaka 2010 alipokwenda akademi ya AFC Eskilstuna ya Sweden, alikocheza hadi mwaka 2011 alipochukuliwa na timu ya vijana ya Mazembe.
Alicheza U-20 ya Mazembe kwa msimu moja kabla ya kupandishwa rasmi timu ya wakubwa mwaka 2012 na moja kwa moja kuwa mchezaji wa kikosi cha kwanza hadi anamaliza Mkataba wake Oktoba mwaka jana.
Ulimwengu alihamia Ulaya baada ya kushinda mataji makubwa akiwa na Mazembe kama Ligi ya Mabingwa Afrika, Super Cup ya Afrika na pamoja na kucheza Klabu Bingwa ya Dunia.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE https://ift.tt/2uIDEsn
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms