Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
KIKOSI cha timu ya taifa ya Tanzania ya soka la ufukweni kimewasili nchini Misri tayari kushiriki Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zinazotarajiwa kufanyika katika mji wa Sharm El Sheikh kuanzia Desemba 8 hadi 14, mwaka huu.
Tanzania inayofundishwa na kocha Boniface Pawasa imepangwa Kundi B pamoja na mabingwa watetezi, Senegal, Nigeria na Libya, wakati Kundi A lina timu za Misri, Morocco, Madagascar na Ivory Coast.
Tanzania itafungua dimba na Libya Jumamosi, yaani Desemba 8, kabla ya kumenyana na Senegal Jumapili (Desemba 9) na kumaliza na Nigeria Jumatatu (Desemba 10).
Wachezaji wa Tanzania wakipata chakula leo mjini Cairo, Misri baada ya kuwasili tayari kushiriki Fainali za Afrika za soka la ufukweni
Nusu Fainali zitafuatia Desemba 12 na Fainali Desemba 14, wakati bingwa na mshindi wa pili watajikatia tiketi ya kwenda kushiriki Fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Paraguay.
Kikosi cha Tanzania kilichowasili Misri leo kinaundwa na; Ibrahim Hamad Abdallah, Juma Sultan Ibrahim, Rolland Narcise Msonjo, Samuel John Mauru, Yahya Said Tumbo, Jaruphu Rajab Juma, Ahmada A Ahmada, Alfa Wilfred Tindise, Kashiur Salum Said, Mohammed Makame Silima, Juma Kaseja Juma na Mbwana Mshindo Mussa.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE https://ift.tt/2RHBqDW
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms