Na Mwandishi Wetu, SONGEA
KLABU ya Azam FC, imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Maji Maji katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara uliofanyika leo mchana kwenye Uwanja wa Majimaji, mjini Songea, Ruvuma.
Sare hiyo inaifanya Azam FC kufikisha pointi 27 na kukaa kileleni kwa muda kwenye msimamo wa ligi ikiisubiri Simba ambayo kama itapata ushindi jioni ya leo itarejea kileleni kwa pointi 29.
Azam FC ndiyo iliyoanza kuliona lango la Majimaji dakika ya 30 kupitia bao safi la winga Joseph Mahundi, aliyeunganisha kiustadi pasi safi ya mshambuliaji Yahya Zayed, bao lililodumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika.
Kiungo wa Azam FC, Frank Domayo akimtoka mchezaji wa Maji Maji leo
Kipindi cha pili Azam FC iliwaingiza nyota kadhaa kwenye dakika tofauti wakiingia viungo Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na mshambuliaji Shaaban Idd, ikiwatoa Bernard Arthur, Salmin Hoza na Idd Kipagwile, mabadiliko ambayo yaliongeza kasi ya mashambulizi wakati timu hiyo ilipokuwa ikishambulia.
Dakika ya 73 Majimaji iliweza kusawazisha bao hilo kupitia kwa Marcel Boniventure, aliyepiga mpira wa moja kwa moja wa kona uliojaa wavuni na kufanya matokeo kuisha kwa sare hiyo.
Kama Azam FC ingekuwa makini ingeweza kujipatia mabao mengine kupitia nafasi walizopoteza kwenye mchezo huo, kipindi cha kwanza kupitia kwa Bernard Arthur, kipindi cha pili ikipoteza nyingine kwa washambuliaji wake Yahya Zayd, Shaaban Idd na beki Yakubu Mohammed.
Mara baada ya mchezo huo, kikosi cha Azam FC kinatarajia kuelekea mkoani Mbeya kesho Ijumaa asubuhi tayari kabisa kwenda kucheza na Tanzania Prisons, mchezo utakaofanyika Uwanja wa Sokoine Jumapili hii.
Kikosi cha Azam FC kilikuwa: Razak Abalora, Himid Mao (C), Bruce Kangwa, Agrey Moris, Yakubu Mohammed, Stephan Kingue, Joseph Mahundi, Salmin Hoza/Shaaban dk 78, Bernard Arthur/Domayo dk 47, Yahya Zayd, Idd Kipagwile/Salum dk 61
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE http://ift.tt/2ESEAO3
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms
Terimakasih anda telah membaca artikel tentang AZAM FC YALAZIMISHWA SARE NA MAJI MAJI SONGEA, 1-1. Jika ingin menduplikasi artikel ini diharapkan anda untuk mencantumkan link https://viralsport.blogspot.com/2018/01/azam-fc-yalazimishwa-sare-na-maji-maji.html. Terimakasih atas perhatiannya.