Na Mwandishi Wetu, MBEYA
TIMU ya Tanzania Prisons imepanda hadi nafasi ya nne kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 2-1 dhidiya Mtibwa Sugar Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Ushindi huo unaifanya timu hiyo ya Jeshi la Magereza ifikishe pointi 36 baada ya kucheza mechi 22 na kusogea nafasi ya nne, ikiishusha Singida United yenye pointi 36 pia za mechi 22, lakini inazidiwa wastani wa mabao.
Mabao ya Prisons yote yamefungwa na beki Salum KImenya, ambaye leo alichezeshwa kama kiungo mshambuliaji na kuonyesha uwezo mkubwa akitikiwsa nyavu dakika za 45 na 49.
Bao pekee la Mtibwa Sugar limefungwa na mshambuliaji Stahmil Mbonde kwa penalti dakika ya 32, kufuatia kiungo Mohammed Issa ‘Banka’ kuangushwa kwenye boksi.
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Ruvu Shooting imelazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Mbeya City Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani.
Singida United imelazimishwa sare 0-0 na Ndanda FC Uwanja wa Namfua mjinio Singida na Maji Maji nayo imetoa sare ya 0-0 pia Lipuli FC Uwanja wa Maji Maji mjini Songea.
Ligi Kuu itaendelea kesho kwa mchezo mmoja, mabingwa watetezi, Yanga wakiwakaribisha Stand United Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
from BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE http://ift.tt/2tA3DF1
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms