
TIMU ya Azam FC imetoka nyuma na kushinda mabao 2-1 dhidi ya wenyeji, Nairobi United katika mchezo wa Kundi B Kombe la Shirikisho Afrika jioni ya leo Uwanja wa Taifa wa Nyayo Jijini Nairobi.
Mshambuliaji Duncan Oluoch alianza kuifungia Nairobi United dakika ya 14, kabla ya mshambuliaji Mkongo, Jephte Kitambala Bola kuisawazishia Azam FC dakika ya 17 na kipa Mghana, Ernest Mohammed akajifunga dakika ya 78 akijaribu kuokoa kuipatia timu ya Tanzania bao la ushindi.
Azam FC inapata ushindi wa kwanza baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo, ikifungwa 2-0 na wenyeji Maniema United huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na 1-0 dhidi ya Wydad Athletics Club ya Morocco visiwani Zanzibar.
Kwa Upande wao Nairobi United wanapoteza mechi ya tatu mfululizo ya Kundi B kufuatia kufungwa 3-0 na Wydad AC Jijini Casablanca na 1-0 nyumbani dhidi ya Maniema United.
Mchezo mwingine wa Kundi B utafuatia Saa 2:00 usiku baina ya Wydad AC na AS Maniema Union Uwanja wa Mohammed V Jijini Casablanca kabla ya timu hizo kurudiana Februari 1 Uwanja wa Martyrs Jijini Kinshasa.
Azam FC inarejea nyumbani kujipanga kwa mchezo wa marudiano na Nairobi United Februari 1 pia Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar.
from BIN ZUBEIRY SPORTS — ONLINE https://ift.tt/4wtM9zW
best mesothelioma law firms, mesothelioma attorneys, mesothelioma
lawyer, mesothelioma lawsuits, mesothelioma lawyers, mesothelioma
lawsuit, mesothelioma attorney, mesothelioma settlement, mesothelioma
lawsuit settlements, mesothelioma settlements, mesothelioma law firm,
lawyer mesothelioma, get a online mesothelioma law firm today,
mesothelioma claims, mesothelioma claim, malignant mesothelioma,
mesothelioma law, mesothelioma law firm california, mesothelioma
compensation, mesothelioma law firms, asbestos settlement, asbestos
claim, mesothelioma, asbestos lawsuit, asbestos lung cancer,
mesothelioma law suit, asbestos claims720, asbestos attorney,
mesothelioma lung cancer, mesothelioma causes, asbestos lawyer390,
mesothelioma cancer, asbestos lawsuits, asbestos lawyers, causes of
mesothelioma, asbestos cancer, mesothelioma law suits, what is
mesothelioma, law offices, mesothelioma symptoms